UNEP imeunda mkakati wa kufikia rasilimali watu ili kuvutia vipaji vya vijana kutoka kwa Nchi Wanachama ambazo zina uwakilishi mdogo na vikundi vya kikanda visivyo na uwakilishi mkubwa. Kumekuwa na kuimarika kwa uanuai kikanda. Kategoria za kitaaluma na makundi yaliopo hapo juu yalishuhudia ongezeko la takriban asilimia 10 ya wafanyakazi kutoka Kundi la Asia ya Pasifiki na takriban asilimia 30 kutoka Kundi la Ulaya Mashariki. Katika mwaka wa 2022, UNEP ilifikia au kushinda kiwango kinacholengwa na Umoja wa Mataifa cha usawa wa kijinsia (asilimia kati ya 47 na 53) katika viwango vyote vya kitaaluma na zaidi.

Is this the pull quote?
No