UNEP imeunda mkakati wa kufikia rasilimali watu ili kuvutia vipaji vya vijana kutoka kwa Nchi Wanachama ambazo zina uwakilishi mdogo na vikundi vya kikanda visivyo na uwakilishi mkubwa. Kumekuwa na kuimarika kwa uanuai kikanda. Kategoria za kitaaluma na makundi yaliopo hapo juu yalishuhudia ongezeko la takriban asilimia 10 ya wafanyakazi kutoka Kundi la Asia ya Pasifiki na takriban asilimia 30 kutoka Kundi la Ulaya Mashariki. Katika mwaka wa 2022, UNEP ilifikia au kushinda kiwango kinacholengwa na Umoja wa Mataifa cha usawa wa kijinsia (asilimia kati ya 47 na 53) katika viwango vyote vya kitaaluma na zaidi.
Chapisho hili linaweza kunakiliwa lote au sehemu yake na kwa namna yoyote kwa madhumuni ya elimu au yasiyokuwa ya biasharaa bila ruhusa maalum kutoka kwa mmiliki wa hakimiliki imradi unaonyesha chanzo chake. Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa litafurahia kupokea nakala ya chapisho lolote linalotumia chapisho hili kama chanzo. Hairuhusiwi kuchapisha chapisho hili ili kuliuza tena au kwa madhumuni mengine yoyote ya kibiashara bila kibali kupitia maandishi kutoka kwa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa. Uteuzi wa mashirika kijiografia katika ripoti hii, na uwasilishaji wa makala humu, haimaanishi utoaji wa maoni ya aina yoyote kwa upande wa mchapishaji au mashirika yanayoshiriki kuhusu hadhi kisheria ya nchi yoyote, kanda au eneo, au ya mamlaka yake, au kuhusu uwekaji wa mipaka yake. Wa Kumtaja: Isipokuwa imeonyeshwa vinginevyo, data yote katika chapisho hili imetolewa kutoka kwa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa. Kwa taarifa zaidi: unep.org/annualreport.
© Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa, 2023