Muungano wa Uendelevu wa Mazingira wa Kidijitali (CODES) - muungano unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ulio na washikadau 1,000 - ulizinduliwa wakati wa Stockholm+50 ili kuunga mkono matumizi ya teknolojia ya kidijitali kushughulikia changamoto za iana tatu kwa sayari. CODES inalenga kuongeza idadi ya nchi na makampuni yanayoshirikiana kutekeleza mipango ya pamoja ya utekelezaji chini ya Mwongozo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Ushirikiano wa Kidijitali.
Chapisho hili linaweza kunakiliwa lote au sehemu yake na kwa namna yoyote kwa madhumuni ya elimu au yasiyokuwa ya biasharaa bila ruhusa maalum kutoka kwa mmiliki wa hakimiliki imradi unaonyesha chanzo chake. Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa litafurahia kupokea nakala ya chapisho lolote linalotumia chapisho hili kama chanzo. Hairuhusiwi kuchapisha chapisho hili ili kuliuza tena au kwa madhumuni mengine yoyote ya kibiashara bila kibali kupitia maandishi kutoka kwa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa. Uteuzi wa mashirika kijiografia katika ripoti hii, na uwasilishaji wa makala humu, haimaanishi utoaji wa maoni ya aina yoyote kwa upande wa mchapishaji au mashirika yanayoshiriki kuhusu hadhi kisheria ya nchi yoyote, kanda au eneo, au ya mamlaka yake, au kuhusu uwekaji wa mipaka yake. Wa Kumtaja: Isipokuwa imeonyeshwa vinginevyo, data yote katika chapisho hili imetolewa kutoka kwa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa. Kwa taarifa zaidi: unep.org/annualreport.
© Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa, 2023