Wakati viongozi wa dunia walipokusanyika katika Kongamano la Umoja wa Mataifa la Mabadiliko ya Tabianchi (COP27) - mkutano wa kimataifa uliofanyika kuimarisha juhudi za kushughulikia hali ya hewa - UNEP ilitoa ripoti mbili kabla ya mazungumzo hayo. Ripoti zote mbili zilichangia kwa Mpango wa Utekelezaji wa Sharm el-Sheikh uliopitishwa na Nchi Wanachama mwishoni mwa kongamano hilo.

Ripoti ya Emissions Gap Mwaka wa 2022: Fursa inayodidimia ilibainisha kuwa ahadi za kushughulikia hali ya hewa zinapelekea ulimwenguni kuelekea kushuhudia kupanda kwa joto kati ya nyuzijoto 2.4 na nyusujoto 2.6 katika karne hii. Mabadiliko ya dharura ya mfumo mzima yanahitajika ili kuweza kufikia nyuzijoto 1.5. Ripoti ilieleza jinsi ya kuleta mabadiliko haya katika sekta ya usambazaji wa umeme, viwanda, uchukuzi na ujenzi, na mifumo ya chakula na ya fedha.

Ripoti ya Kukabiliana na Pengo la Uzalishaji wa Gesi Chafu ya Mmwaka wa 2022:Hatua Ndogo, Mwendo wa Konokono ya UNEP ilibainisha kuwa ufadhili na utekelezaji wa hatua za kukabiliana na hali kutegemea eneo hazitoshi. Kati ya dola za Marekani bilioni 160 na bilioni 340 zitahitajika kwa mwaka kukabiliana na hali kutegemea eneo kufikia mwaka wa 2030. Mwaka wa 2020, mtiririko wa fedha za kimataifa za kukabiliana na hali kwa nchi zinazoendelea ulikuwa dola za Marekani bilioni 29 tu.

Tags
Image
Picha: UNEP
Number of columns
One
image credit color
white