Mfuko wa kushughulikia mifumo ya ekolojia duniani kutegemea eneo (EbA), unaosimamiwa na UNEP kwa ushirikiano na Muungano wa Kimataifa wa Kuhifadhi Mazingira, hutoa mtaji wa kuanzisha kampuni kupitia mbinu bunifu za EbA. Mchakato wa kwanza na wa pili wa uteuzi wa wanaopokea ruzuku ya Mfuko wa EbA Duniani uliidhinisha dola za Marekani milioni 5.6 kwa miradi 23, ambazo zitasaidia mifumo ya ekolojia kote duniani, ikiwa ni pamoja na kutunza miamba ya matumbawe nchini Ufilipino na kurejesha kingo za mito ili kudhibiti mmomonyoko wa udongo nchini Fiji. Mchakato wa uteuzi wa tatu na wa nne wa wanaruzuku unaendelea, na miradi mingine 30 ikitarajiwa kuanza.

Wakati uo huo, orodha ya fedha zinazowekwa kwa faida ziliongezeka na kuwa zaidi ya miradi 45, ikijumuisha mradi wa dola milioni 6 nchini Msumbiji kutunza ukanda wa pwani kupitia uboreshaji na uhifadhi wa mazingira. Kwa ujumla, miradi ya UNEP ya EbA inalenga kurejesha hekta 131,000 za mifumo ya ekolojia na kunufaisha watu milioni 2.7.

Tags
Image
Utunzaji wa miamba ya matumbawe ni sehemu muhimu ya programu za UNEP za kushughulikia mifumo ya ekolojia kwa kuzingatia eneo.
Number of columns
One
image credit color
white