20 November 2023 Ripoti

Ripoti ya Pengo la Uzalishaji wa Gesi Chafu Mwaka wa 2023

Waandishi: UNEP
Jalada

Kadiri athari mbaya kwa hali ya hewa zinavyozidi kuongezeka, ongezeko la joto kushuhudiwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kuongezeka, Ripoti ya Pengo la Uzalishaji wa Gesi Chafu Mwaka wa 2023: Rekodi iliyovunjwa – Ongezeko la joto lilizidi zaidi, ila dunia imeshindwa kupunguza uzalishaji wa hewa chafu (tena) inaonyesha kuwa ulimwengu unaelekea kushuhudia ongezeko la joto kuliko katika malengo ya Mkataba wa Paris iwapo nchi hazitachukua hatua zaidi kuliko zilivyoahidi.  Ripoti hii ni toleo la 14 katika msururu unaowaleta pamoja wengi wa wanasayansi wa mazingira duniani kuchunguza mielekeo ya siku zijazo ya uzalishaji wa gesi ya ukaa na kutoa masuluhisho yanayowezekana kwa changamoto za ongezeko la joto duniani.

Mambo mapya katika ripoti ya mwaka huu 

Ripoti hii inaonyesha kuwa kuna hatua ambazo zimepigwa tangu Mkataba wa Paris ulipotiwa sahihi katika mwaka wa 2015. Uzalishaji wa gesi ya ukaa kufikia mwaka wa 2030 kwa kuzingatia sera zilizopo ulikadiriwa kuongezeka kwa asilimia 16 wakati wa kupitishwa kwa mkataba huu.  Leo, makadirio ya ongezeko ni asilimia 3. Hata hivyo, makadirio ya uzalishaji wa gesi ya ukaa kufikia mwaka wa 2030 bado ni sharti yapungue kwa asilimia 28 ili kufikia malengo ya Mkataba wa Paris ya nyuzijoto 2 na kwa asilimia 42 ili kufikia nyuzijoto 1.5.

Mambo yakisalia jinsi yalivyo, utekeleza kikamilifu wa Ahadi Zinazowekwa na Taifa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris utawezesha ulimwengu kudhibiti ongezeko la joto hadi nyuzijoto 2.9 zaidi kuliko viwango vya kabla ya viwanda. Utelelezaji kikamilifu wa NDC zilizo na masharti unaweza kupunguza hadi nyuzijoto 2.5.

Ripoti hii inatoa wito kwa mataifa yote kuharakisha hatua za mabadiliko ya kupunguza hewa ya ukaa wakati wa maendeleo kwa uchumi wote. Nchi zilizo na uwezo mkubwa na huchangia zaidi kwa uzalishaji wa hewa chafu zitahitaji kuchukua hatua kabambe na kusaidia mataifa yanayoendelea yanapofanya juhudi za kupunguza hewa ya ukaa wakati wa kukuza uchumi.

Ripoti hii inaangazia jinsi utekelezaji madhubuti wa unavyoweza kuimarisha awamu inayofuata ya NDC ambazo nchi zinapaswa kuwasilisha katika mwaka wa 2025, ili kupunguza uzalishaji wa gesi ya ukaa kufikia mwaka wa 2035 kurandana na viwango vya chini ya nyuzijoto 2 na nyuzijoto 1.5. Inaangazia pia uwezo na madhara ya mbinu za Uondoji wa Kaboni Dioksidi kama vile masuluhisho yanayotokana na mbinu za kiasili kunasa na kuhifadhi hewa ya ukaa moja kwa moja.

Ripoti ya Pengo la Uzalishaji wa Gesi Chafu

Ripoti ya Pengo la Uzalishaji wa Gesi Chafu ni ripoti kuu ya UNEP inayotolewa kila mwaka kabla ya mazungumzo ya kila mwaka kuhusu Mazingira. EGR hufuatilia pengo kati hali ya uzalishaji wa hewa chafu duniani na ahadi zilizotolewa na nchi kwa sasa na hali inavyopaswa kuwa ili kud ongezeko la joto lisizidi nyuzijoto 1.5. Kila toleo huchunguza njia za kuziba pengo la uzalishaji wa hewa chafu.

Mataifa ni sharti yaimarishe juhudi zaidi ya ahadi za Paris au yakabiliwe na ongezeko la joto duniani la nyuzijoto kati ya 2.5 na 2.9

Huku hali ya joto duniani na uzalishaji wa gesi ya ukaa vinapovunja rekodi, Ripoti ya hivi punde ya Pengo la Uzalishaji wa Hewa Chafu kutoka kwa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) inaonyesha kuwa ahadi zilizopo chini ya Mkataba wa Paris zitafanya ulimwengu kushuhudia joto la nyuzijoto kati 2.5 na 2.9 zaidi ya viwango vya kabla ya viwanda katika karne hii, hali…

Wito wa kuweka ripoti mpya za kushughulikia mazingira

Binadamu wanavunja rekodi mbaya sana kuhusiana na mabadiliko ya tabianchi. Uzalishaji wa gesi ya ukaa na wastani wa joto duniani  inaendelea kuongezeka huku matukio mabaya ya hewa yakitokea mara kwa mara, kuongezeka kwa kasi na kuwa mabaya zaidi.