Kaulimbiu ya jumla ya UNEA-6 ni juhudi madhubuti, jumuishi na endelevu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa bayoanuai na uchafuzi.

Nchi Wanachama na washikadau watakuja pamoja kwa UNEA-6 kujadili kuhusu jinsi ya kuendeleza Muongo wa Kuchukua Hatua kwa kuzingatia ushughulikiaji wa maingiliano ya changamoto za mazingira za aina tatu duniani. Msururu wa mijadala ya viongozi na  na washikadau mbalimbali na zaidi ya hafla rasmi 30 za kando nahafla nyinginezo za aina hii   zinatarajiwa kuweka misingi ya siku zijazo wa kuimarishwa kwa juhudi za uratibu wa kimataifa na kikanda na Umoja wa Mataifa, Nchi Wanachama na wabia ili kuchukua hatua zangazi ya juu za kushughulikia sayari.

  • Katika aya ya 9 ya uamuzi wa 5/4 wa UNEA, Baraza liliomba Ofisi yake, kwa kushauriana na Kamati ya Wawakilishi wa Kudumu, kufafanua kaulimbiu ya UNEA-6 kabla ya miezi kumi na miwili kabla ya mkutano.
  • Wakati wa mkutano wa pamoja wa Ofisi ya Baraza na Kamati ya Wawakilishi wa Kudumu tarehe 30 Januari mwaka wa 2023, Ofisi iliamua kaulimbiu ya UNEA-6.
  • Rais wa UNEA-6 alituma barua tarehe 6 Februari mwaka kwa Mawaziri wa Mazingira ili kuwajulisha kuhusu kaulimbiu.

Pitia sayansi, sera na hatua za kushughulikia changamoto za aina tatu za mazingira duniani:

WHEN:
26 Feb 2024 - 1 Mar 2024
WHERE:
Nairobi, Kenya

Pakua aouu rasmi ya UNEA

Pata atiba za vikao, matangazo, ramani na taarifa kwa wakati halisi popote ulipo. Pakua apu ya UNEA kwa kutumia kifaa kilichopo hapo chini.

Android

iOS