• Maelezo ya Jumla
  • Mkutano wa Kilele Barani Afrika
  • Hafla za Kufuatilia Hatua
  • Hafla Zinazohusiana na UNEP
  • Hafla za Kando za UNEP

Lini: Septemba 4-8 , 2023

Wapi: Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyatta (KICC), Nairobi, Kenya.

Usajili umefungwa.

Wiki ya Tabianchi barani Afrika (ACW) ni hafla ya kila mwaka ambayo huleta pamoja viongozi kutoka serikalini, mashirika ya biashara, mashirika ya kimataifa na mashirika ya uraia kutafuta njia za kupunguza uzalishaji wa gesi ya ukaa huku wakikabiliana na janga la mabadiliko ya tabianchi. Mwaka huu, ACW 2023 itafanyika kuanzia tarehe 4 hadi 8 Septemba jijini Nairobi, Kenya, ikiongozwa na Serikali ya Kenya.

ACW 2023 itaandaliwa sambamba na Mkutano wa Kilele wa Tabianchi wa Afrika utakaoanza tarehe 4 hadi 8 Septemba jijini Nairobi, Kenya, pia utakaoongozwa na Serikali ya Kenya. Wakati wa ACS, viongozi barani Afrika watatakiwa kutoa ahadi kabambe na kujitolea kuzitekeleza ili kupitisha "Mwongozo wa Ahadi na Kujitolea Kuzitimiza."

Mojawapo ya wiki nne ya Kikanda ya Mazingira iliyofanyika mwaka huu, ACW 2023 inaimarisha kasi tunapoelekeaKongamano la Umoja wa Mataifa la Mabadiliko ya Tabianchi la COP 28mjini Dubai na kuhitimishwa kwa tathmini ya kwanza ya kimataifa, liyoundwa ili kupanga njia ya kutimiza malengo ya Mkataba wa Paris na kumakinikia michango ya kanda wakati wa kutoa tathmini ya Kimataifa. 

ACW 2023 itawekwa katika makundi manne kimfumo, kila moja wapo ikiangazia mada mahususi: 

  • Mifumo na sekta ya nishati  
  • Miji, makazi ya mijini na vijijini, miundomsingi na uchukuzi  
  • Ardhi, bahari, chakula na maji 
  • Jamii, afya, riziki, na uchumi  2023.     

ACW 2023 imeandaliwa na Mkataba wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC), Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) na Benki ya Dunia, kwa msaada wa wabia wa kikanda: Umoja wa Afrika (AU)Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi wa Afrika (ECA)naBenki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Wawakilishi kutoka UNEP watapanga/kushiriki katika hafla kama ilivyoainishwa kwenye vitufe husika.  Saa za eneo:  Masaa ya Afrika Mashariki (EAT)

Pitia programu kamili ya ACW 2023.

 

Africa Climate Summit bannerPicha: Mkutano wa Kilele Barani Afrika

Wakati wa Mkutano wa Kilele wa Tabianchi wa Afrika(ACS), utakaendelea kuanzia tarehe 4 hadi 9 Septempa huku Serikali ya Kenya ikiwa mwenyeji, viongozi watatakiwa kutoa ahadi kabambe na kujitolea kuzitekeleza ili kupitisha "Mwongozo wa Ahadi na Kujitolea Kuzitimiza."

Wawakilishi kutoka UNEP watapanga/kushiriki katika hafla zifuatazo wakati wa Mkutano wa Kilele wa Tabianchi wa Afrika.  Saa za eneo:  Masaa ya Afrika Mashariki (EAT)

Hafla za Ngazi ya Juu:

Septemba 3, mda utatolewa | Mazungumzo ya Ngazi za Juu Ya Mawaziri kuhusu Kuimarisha Ushugulikiaji wa Hali na Ufadhili katika Mkutano wa Kilele wa Tabianchi

Septemba 4, 3:30-4:30 pm| Hafla Ya Ngazi Ya Juu wakati wa Mkutano wa Kilele wa Tabianchi wa Afrika - Changamoto ya Maji Safi

Septemba 6, 10:00-11:00 am| Punguza Joto Barani Afrika: Kuimarisha Masuluhisho Endelevu ya Kupunguza Joto ili kuwa Bara Linalostahimili Hali ya Mazingira

Hafla Zinazohusiana na UNEP

​Septemba 5, 1:30-3:30 pm Wanawake na Mabadiliko ya Nishati

 

Wawakilishi kutoka UNEP watapanga/kushiriki katika hafla zifuatazo wakati wa Wiki ya Tabianchi barani Afrika.  Saa za eneo:  Masaa ya Afrika Mashariki (EAT)

Hafla za Kufuatilia Hatua

Septemba 7, 09:00-10:15 am | Kutumia uwezo wa Afrika wa nishati endelevu: changamoto, fursa, na uvumbuzi

Septemba 7, 10:30-11:30 am | Madini Muhimu ili kuwa na Mabadiliko ya Haki ya Nishati Isiyochafua Mazingira

Septemba 7, 2:00-3:15 pm | Kukuza mustakabali endelevu: Kutumia uwezo wa Afrika katika sekta ya ujenzi

Septemba 7, 4:45-6:00 pm| Masuluhisho Jumuishi ya Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi Kukuza Hatua, Ufadhili, na Sera ya Vijana

Septemba 8, 09:00-10:15 am | Kukuza mfumo wa miundomsingi thabiti isio na gesi ya ukaa barani Afrika: wajibu wa uchukuzi​

Septemba 8, 2:45-4:00 pm| Uhusiano kati ya afya na mabadiliko ya Tabianchi: Kuimarisha jhatua kupitia mfumo jumuishi wa tabianchi na juhudi za hewa safi barani Afrika

Wawakilishi kutoka UNEP watapanga/kushiriki katika hafla zifuatazo wakati wa Wiki ya Tabianchi barani Afrika.  Saa za eneo:  Masaa ya Afrika Mashariki (EAT)

Hafla Zinazohusiana na UNEP

Septemba 4-5 | Kukuza Matumizi ya Tena na Tena katika NDCs - Nyenzo za vitendo (warsha ya siku mbili

Septemba 5-7 | Jukwaa la Kikanda la CTCN la NDE za Mfumo wa Teknolojia (warsha ya siku 3)

​Septemba 5, 1:30-3:30 pm | Wanawake na Mabadiliko ya Nishati (hafla ya Mkutano wa Kilele wa Tabianchi wa Afrika)

Septemba 6, 2:00-3:30 pm | Kutumia Masuluhisho ya Kiasili Kushughulikia Mazingira barani Afrika

Hafla ya Kuchukua Hatua

Septemba 4, 3:00 pm | Ubia wa Kutumia Nishati ya Jua: Kubadilisha majumba katika nchi zinazohifadhi wakimbizi barani Afrika kufikia mwaka wa 2027

Septemba 4, 3:30-4:30 pm | Masuluhisho ya Kutegemewa ya Ustahimilivu wa Miamba ya Matumbawe kwa Kenya na Tanzania

Septemba 6, wakati utatolewa | Soko la Ufanisi wa Malengo - Kuwekeza katika ufanisi wa nishati ili kusaidia mustakabali wa Afrika wa bei nafuu bila kuchafua mazingira

Septemba 6, 2:00-3:00 pm | Mitazamo ya vijana wa UNICEF na UNEP: masuluhisho kwa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watoto na vijana

Septemba 6, 3:30-4:30 pm| Tathmini: Kuanzia kwa Mahitaji ya Teknolojia hadi kwa Utekelezaji

Septemba 7, 10:30-11:30 am| Kukusanya fedha za ufadhili wa mazingira kupitia mifumo bunifu ya biashara na ufadhili ili kuwa na mabadiliko kidigitali nchini Ghana

Septemba 7, 12:00-1:00 pm| Hatua za Kushughulikia Mazingira kwa Kipato Barani Afrika: Kupunguza Pengo na Kuimarisha Ushirikiano

Septemba 7, 12:00-1:00 pm | Kutumia Masuluhisho ya Kiasili ili uwa na Mabadiliko ya Kushughulikia Mazingira barani Afrika

Septemba 7, 1:30-2:30 pm | Mazingira kama nguzo ya Masuluhisho ya Tabia na Bayoanuai

Septemba 7, 3:00-4:00 pm | Kuunga mkono juhudi za Afrika za kupunguza uzalishaji wa methani - Hatua za Kutimiza Ahadi ya Kimataifa ya Methani

Septemba 8,  09:00-10:00 am | Miji endelevu ni jamii zinazostawi: kubadilisha miji barani Afrika kupitia kushughulikia mazingira

Septemba 8, 0900-1100 am | Kuchunguza Matumizi ya Akili Unde Kushughulikia Mazingira Barani Afrika 

Septemba 8, 10:30-11:30 pm | Kukabiliana na changamoto za madeni, maendeleo na mazingira: Wajibu wa bajeti endelevu

Septemba 8, 12:30-1:30 pms | Kutumia Mikakati ya Utekelezaji wa Kitaifa (NAPs) kuimarisha kukabiliana na hali kupitia rasilimali za maji

Septemba 8, 12:30-2:30 pm | Kubuni na Kumarisha Mifumo ya Kitaifa ya Uvumbuzi ya Kushughulikia Mazingira

Septemba 8, 4:30-5:30 pm| Mifumo ya Mazingira, Amani na Chakula: Kuimarisha Masuluhisho Thabiti Barani Afrika