Urejeshaji na utunzaji wa mifuo muhimu ya ekolojia

Muongo wa Umoja wa Mataifa wa Kuboresha Mifumo ya Ekolojia, unaosimamiwa na UNEP na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), unasaidia kutekeleza ahadi za kuboresha hekta bilioni 1 za ardhi, eneo lenye ukubwa sawa na China, kufikia mwaka wa 2030. Mwaka wa 2022, Muongo huo ulituza Miradi 10 za kwanza Anzilishi za Kuboresha Mifumo ya Ekolojia Duniani, zinazolanga kuboresha zaidi ya hekta milioni 68 - eneo kubwa kuliko Myanmar, Ufaransa au Somalia - na kubuni nafasi za kasi takribani milioni 15.

Mpango mpya wa kimataifa wa kuishi kwa amani na mazingira

Katika mwezi wa Desemba, katika Kongamano la Umoja wa Mataifa la Bayoanuai (mkutano wa 15 wa Kongamano la Nchi Wanachama wa Mkataba wa Uanuai wa Kibayolojia - COP15), Mataifa yalikubaliana juu ya mfumo mpya msingi wa kutunza bayoanuai - Mfumo wa Kimataifa wa Bayoanuai wa Kunming-Montreal, ukiwa na malengo manne na shabaha 23 za kupunguza uharibifu wa bayoanuai kufikia mwaka wa 2030. Shabaha - ambazo nyingi zinalenga kuimarisha haki za watu wa kiasili, ambao ni wasimamizi wakuu wa bayoanuai - ni pamoja na:

Kuimarisha juhudi za kukabiliana na uzalishaji wa methani

Katika mwaka wake wa kwanza, Kituo cha Kimataifa cha Kufuatilia Uzalishaji wa Methani Duniani (IMEO) cha UNEP kilitekeleza wajibu muhimu kusaidia kupunguza uzalishaji wa methani, kichocheo cha pili kwa ukubwa cha ongezeko la joto duniani. Kituo hiki kilianzishwa ili kusaidia kufikia malengo kama vile Ahadi za Methani Duniani za kupunguza asilimia 30 ya uzalishaji wa methani katika sekta ya mafuta na gesi, sekta ya kilimo na taka kufikia mwaka wa 2030.